Makala - Kilimo cha Mboga Mboga
![]() |
Mti wa Bilinganya |
UANDAAJI WA KILIMO CHA MBOGA MBOGA
Kilimo
ni hazina katika nchi yoyoe mali hiyo ina manufaa kwa mtu binafsi na kwa taifa kwa ujumla.Nchi yetu ya Tanzania ina kilimo cha
aina nyingi ,baadhi ya vilimo hivyo ni vya mboga mboga na matunda na chakula.
Hii
leo tunakuletea kilimo cha mboga mboga
hasa tunaangazia zaidi kilimo cha mchicha,kabichi na Chinese ambavyo ndivyo
vinatajwa nqa wtu wengi kuwa ndiyo mboga maarufu na inzaalishwa kwa wingi katika nchi ya Tanzania.
Tunaanza
na zao la mchicha,Mchicha ni zao ambalo
hulimwa kwa wingi sehemu yenye udongo wa ufinyanzi na utifutifu kwa mkoa
wetu wa Morogoro hasa Morogoro mjini zao
la mchicha hulimwa sana maeneo ya mji mpya,kichangani na maeneo mengine ambayo
yamepitiwa na mito au sehemu nyingine zenye maji mengi.
Mchicha
umegawanyika katika sehemu kuu mbili nazo
ni mchicha wa asili na mchicha wa kupandwa,Mchicha wa asili ni ule ambao
umeota bila kupandwa na mwanadamu ambao jina lake maarufu huitwa mchicha bwasi na
mchicha uliopandwa na mwanadamu umegawanyika katika makundi tofauti upo unaoota
baada ya siku saba na siku tano.
Mchicha
ambao majani au maua yake hutumika kama chakula hutibu magonjwa yafuatayo kuuma
mgongo,unatibu figo,tezi shingo,kusafisha njia ya mkojo,kusafisha damu,dawa ya
kikohozi na inasaidia kupata haja kubwa kwa wingi .
Msomaji
wa makala hii nakushauri sana utumie mboga hii ya mchicha kwa ajili ya
kuimarisha afya yako ili uweze kuwa mtu makini katika taifa hili,pia tutunze
vizuri ardhi yetu na vyanzo vya maji kwa ajili ya kuweza kustawisha mboga
zilizo bora kwa manufaa ya watu walio sasa na baadae hiko ndicho kilimo cha
mchicha hiyo ndiyo mboga bora kwa
mwanadamu.
Kabichi
ni zao ambalo ustqawi zaidi katika mikoa ya Arusha,Kilimanjaro,Morogoro,Tanga,Iringa na
Mbeya.kabichi ina madini aina ya chokaa,protini na maji kwa wingi ,mboga hii
inaweza kuliwa bila kupikwa au kuchemshwa kwa kutengenezwa kachumbari pia
inaweza kupikwa pamoja na vyakula kama vile mahargwe na nyama.
Kabichi
ni zao ambalo upendelea zaidi hali ya baridi zao hili hustawi na kutoa mazao mengi na bora zaidi kwenye sehemu zenye miinuko ya kuanzia mita
1200 hadi 1900 kutoka usawa wa bahari zao hili ustawi zaidi katika udongo wa
kitifutifu na wenye rutuba nyingi na uwezo wa kuhifadhi unyevu kwa muda mwingi vilevile
linaweza kustawi katika aina mbalimbali za udongo ilimradi udongo huo
usitwamishe maji na usiwe na chumvi nyingi.
Endapo
udongo hauna rutuba ya kutosha uongezewe mbolea za asili kama mbolea ya samadi
na vunde,kabichi zinazolimwa hapa Tanzania ni prize druntied ambayo vichwa
vyake ni vikubwa kilo 2 mpaka kilo 2 na nusu na ni bapa ambayo huchelewa
kukomaa siku 110 hadi 120 tangu kupandikiza miche na hupasuka kirahisi aina hii
huvumilia hali jua kali
Copenhagen
market,vichwa vyake ni vya mviringo na hupasuka kirahisi aina hii pia hukomaa
mapema siku 90 hadi 100 tangu kupandikiza miche
Groly
of enkhiuzen,vichwa vyake ni vya mviringo hii huvumilia hali ya jua kali lakini
huchelewa kukomaa siku 100 hadi 120 tangu kupandikiza miche na havumilii hali
ya kupasuka.Aina nyingine ni Brunswick na Danish ball head.
Kabichi
ni zao linalotumia virutubisho vingi aridhini kulinganisha na mboga
zingine.Hivyo kabla ya kustawisha panda mazao jamii ya mikunde ili kuongeza
rutuba,Halikadhalika baada ya kuvuna panda mazao yanayotumia chakula kidogo
kama vile karoti hubadilisha mazao pia hupunguza kuenea kwa wadudud waharibifu
na magonjwa.
Mbegu
za kabichi huanza kuoteshwa kitaluni na baadae miche huamishiwa shambani ,lima
vizuri sehemu itakayooteshwa mbegu,weka mboleaza asili zlizooza vizuri kiasi
cha ndoo 5 hadi 10 zenye ujazo wa lita 20 kwa eneo la mita mraba 10.Changanya
vizuri mbolea na udongo kasha lainisha udongo kwa kutumia reki.Baada kulainisha
udongo tengeneza tuta lenye nafasi ya sentimita 10 mpaka 15 kutoka mstari hadi
mstari.
Funika
mbegu kwa udongo au mbolea laini kasha tandaza nyasi kavu ili kuhifadhi
unyevu,mwagilia maji kila siku asubuhi na jioni mpaka mbegu zitakapoota ,miche
huwa tayari kwa kupandikizwa shambani baada ya majuma 3 hadi 5 tangu kuoteshwa.
Kabichi
hukomaa na kuvunwa baada ya siku 60 hadi 120 kutegemea aina iliyostawishwa
tangu kupandikizwa miche.
Chinese
ni moja kati ya mazao ya mboga mboga inayolimwa sana nchi Tanzania,asili yake
ni China na baadae ikasambaa dunia nzima.Chinese inakuwa vizuri kwenye jotolidi
18 hadi 22,zao hili linategemea maji mengi wakati wa ukuaji na linakua vizuri
kwenye udongo wa kichanga na wenye unyevunyevu wa kutosha,wakati unaandaa
shamba udongo utifuliwe vizuri kabla ya kupanda na andaa shamba wiki 6 kabla ya
kupanda .
Jinsi
ya kuandaa kitalu kinatakiwa kiwe na upana wa mita 1 na urefu wa mita 5.Kitalu
kinatakiwa kiwe na kingo ili kuzuia maji kutoka nje ya kitalu kasha panda mbegu
kwenye kitalu kwa sentimita 15 hadi 20 mstari hadi mstari.
Tumia
mbolea ya kuku,mbuzi na nguruwe,tumia ndoo katika kila kitalu chenye mita 5 na
pia weka mbolea ya
Kukuzia
ya UREA kwa kila kitalu pale mmea unapofikia majani 5.Chinese hukoo baada ya
miezi 3 hadi 4 inategemea na aina.Vuna
kwa kutumia kisu au mkono,maisha ya Chinese ni mafupi sana tofauti na mboga
zingine,hivyo unatakiwa kusafisha na pia baada hapo unaweza kutunza kwenye
friji ili kuzuia kukauka.na hizo ndizo mboga mboga zinazosababisha mwanadamu
kukua vizuri bila kupatwa na magonjwa.
![]() |
Mboga aina ya kabichi |
Comments
Post a Comment